+255 222215701   info@mloganzila.or.tz



Watumishi wa Maabara MNH-Mloganzila watakiwa kujituma zaidi

Oct 21 2022

Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Tiba Shirikishi Hospitali ya Taifa Muhimbili - Mloganzila, Dkt. Lulu Sakafu ( wakwanza kushoto ) akizungumza na wataalamu wa maabara .



Watumishi wa maabara wakiwa kwenye kikao hicho.



Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Tiba Shirikishi Hospitali ya Taifa Muhimbili - Mloganzila, Dkt. Lulu Sakafu amewahimiza watumishi wa Idara ya Maabara kufanya kazi kwa kujituma na kutatua changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao ili kufanikisha utoji huduma bora kwa wateja.

Akizungumza na watumishi wa Idara ya Maabara, Dkt. Sakafu amesisitiza kuwa iwapo kila mtu atawajibika katika eneo lake itasaidia kufanya vipimo vingi na kutoa majibu kwa wakati na hivyo kuendelea kujenga imani kwa wateja sambamba na kuvutia hospitali nyingine kuleta sampuli katika Maabara  ya Mloganzila.

Mnapaswa kufanya kazi kwa nidhamu, kujituma na kuhakikisha muda wote mnakuwa kazini na kutekeleza majukumu yenu bila kushurutishwa au kukumbushwa” amesema Dkt. Sakafu.

Pamoja na hayo, Dkt. Sakafu ameongeza kuwa kila mtumishi atatakiwa kuwa na malengo ya utendaji kazi yanayopimika na atapimwa kupitia malengo hayo hivyo itakuwa rahisi kutambua uwajibikaji wa kila mmoja katika idara.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Maabara Dkt. Flora Ndobho amewashauri watumishi hao kuendelea kufanya kazi kwa umoja (team work) na kutekeleza maelekezo yanayotolewa na viongozi nyakati zote.

Kikao hiki ni muendelezo wa vikao vya idara vyenye lengo la kujipanga na kuweka mikakati ya kuboresha huduma zinazotolewa na Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila.