LOADING...
Jan 10 2023
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila Bi. Zuhura Mawona akizungumza na wauguzi wakati wa kikao kilicholenga kujadili changamoto zinazoikabali kada hiyo pamoja na namna bora ya kuboresha mazingira ya utendaji kazi wao ili kuweza kuhudumia wagonjwa bila vikwazo vyovyote.
Wauguzi wakiwa katika kikao hicho
Wauguzi wakiwa katika kikao hicho
Wauguzi wakiwa katika kikao hicho
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila Bi. Zuhura Mawona amewataka wauguzi kujenga tabia ya kujiendeleza kielimu Ili kuongeza ujuzi kwa kuwa lengo la hospitali ni kutoa huduma iliyo bora na inayoenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia.
Bi. Zuhura ameyasema hayo wakati wa kikao kilichohusisha wauguzi kutoka idara mbalimbali hospitalini hapo ambacho kilicholenga kujadili changamoto zinazoikabali kada hiyo pamoja na namna ya kuboresha mazingira ya utendaji kazi wao ili kuweza kuhudumia wagonjwa bila vikwazo vyovyote.
"Teknolojia kila siku inazidi kukuwa na vitu vipya vinagundulika hivyo ni wajibu wa kila muuguzi kujiendeleza kitaaluma ili kuendeana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia" ameeleza Bi Zuhura
Bi. Zuhura amewataka wauguzi kuzingatia kanuni na taratibu za taaluma yao na kufanya kazi kwa ushirikiano na kila mtu kwa nafasi yake awe tayari kutoa ushauri, kupokea na kuomba ushauri pale inapohitajika kwa kuwa lengo lao ni kutoa huduma iliyobora kwa jamii.
Amesisitiza kuwa sehemu kubwa ya huduma ya afya inategemea wauguzi, na taaluma ya uuguzi ni taaluma inayosomewa na inaongozwa na kanuni, hivyo kila muuguzi anapaswa kutoa huduma kwa kuzingati kanuni zilizowekwa na hapaswi kutoa huduma ambayo haijui na hana taaluma nayo.