LOADING...
Apr 2 2019
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa kushirikiana na kampuni ya dawa ya Roche ya nchini Kenya imeandaa mkutano wa kisayansi wa kuwajengea uwezo wataalam wa Radiolojia, Pathiolojia, Upasuaji, tiba ya mionzi na dawa kufanya upasuaji wa saratani ya matiti kwa kutoa uvimbe bila kuondoa titi lote kwa wagonjwa wenye dalili za mwanzoni.
Mkutano huo wa kisayansi ambao ni wa kwanza kufanyika katika Hospitali ya Mloganzila umefunguliwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili Prof. Lawrence, umelenga kukumbushana namna bora ya kuwapatia matibabu kwa njia ya kisasa wagonjwa ambao wamethibitika kuwa na saratani ya matiti.