LOADING...

+255 222215701   info@mloganzila.or.tz



Serikali ya Zanzibar kujenga hospitali mithili ya Mloganzila

Mar 14 2019

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) inatarajia kujenga hospitali kubwa ya kisasa yenye uwezo wa kubeba vitanda 1,000 ili kutoa huduma pamoja na kufundishia watalaam wa fani mbalimbali za afya.
 

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar, Bi. Asha Ali Abdulla alipotembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa lengo la kujifunza na kupata uzoefu juu ya uendeshaji wa hospitali hiyo.