+255 222215701   info@mloganzila.or.tz



Dkt. Magandi: Wataalamu tarajali hudumieni wananchi kama ambavyo mngetamani kuhudumiwa.

Dec 13 2022

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Julieth Magandi akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo elekezi kwa wataalamu wapya, tarajali na wakujitolea yaliyofanyika Mloganzila.

Baadhi ya wataalamu tarajali wakifatilia mafunzo hayo kwa makini.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano MNH-Mloganzila Bi. Sophia Mtakasimba akiwasisitiza wataalamu hao kuzingatia maadili ya kazi na kutunza siri za wagonjwa.

Baadhi ya wakurugenzi waliohuzuria mafunzo hayo wakifatilia mada zinazowasilishwa kwa makini.

Afisa wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) Bi. Sheila Mlembe akiwasisitiza wataalamu hao kufanya kazi na kuepukana na maswala ya Rushwa mahala pa kazi.

Dkt. Magandi akifatilia mafunzo hayo

Baadhi ya wataalamu tarajali wakifatilia mafunzo hayo kwa makini.

Wataalamu tarajali na wa kujitolea wametakiwa kutoa huduma bora na upendo kwa wateja kwa kuwa dira ya Hospitali kwa sasa ni kutoa huduma ambazo zitakidhi matarajio ya wananchi.
hospitali imejikita katika kutoa huduma bora na zinazokidhi matarajio kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na  Naibu Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Dkt. Julieth Magandi wakati wa ufunguzi wa mafunzo elekezi kwa watumishi wapya, tarajali na wale wanaojotolea.

Dkt. Magandi ameongeza kuwa uongozi wa hospitali umejitahidi kuboresha huduma  ili kujenga imani kwa wananchi pamoja na kuifanya Hospitali ya Mloganzila kuwa kimbilio la kupata huduma za afya hapa nchini.

“Wakati unamhudumia mgonjwa hebu vaa viatu vyake na kujiuliza, huduma hii ninayoitoa hapa ningekuwa natendewa mimi au ndugu yangu wa karibu ningeridhika nayo?, ukijiuliza hivyo hakika utamuhudumia vizuri mgonjwa aliyeko mbele yako” amesema Dkt. Magandi.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Masiliano MNH-Mloganzila, Bi. Sophia Mtakasimba amewataka watumishi hao kuzingatia maadili ya kazi kwa kutunza siri za wagonjwa kwani kitendo cha kutoa nje siri za wagonjwa  kinapoteza imani kwa wagonjwa au ndugu wanaotaka kuwaleta ndugu zao hospitalini hapa

Akitoa mada kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, Afisa wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Ubungo, Bi. Sheila Mlembe amewataka watumishi hao kutoa huduma kwa wananchi bila upendeleo wowote na bila kuomba au kutengeneza mazingira ya rushwa.

Bi. Sheila amesema TAKUKURU imeamua kutoa mafunzo hayo kwa watumishi kwa lengo la kujenga kizazi chenye maadili na kisichotumia nafasi zao vibaya kwa lengo la kujinufaisha.

Katika mafunzo hayo yaliyohusisha watumishi 183 kutoka kada mbalimbali ikiwemo Madaktari 73, Wauguzi 55, Wataalamu wa Radiolojia 4, Wafamasia 12, Wataalam wa Maabara 11 na watumshi wa kujitolea 28, ambapo mada mbalimbali zimewasilishwa ikiwemo maadili ya utumishi wa umma, mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI mahala pa kazi, huduma bora kwa wateja na mapambano dhidi ya rushwa.